Wakati fulani tunakutana na majaribu, matatizo, shida na vikwazo kiasi cha kudhani hakuna njia nyingine ya kutuwezesha kusonga mbele. Leo naomba nikukumbushe kuwa Mungu hufanya njia na kuleta suluhisho wakati ambapo huonekana kama hakuna kabisa njia au suluhisho.
Mungu siku zote huleta utatuzi kwa tatizo lolote tunalokutananalo na kufanya mlango kwa jaribu lolote linalotupata kwa kuridhia kwake (1 Wakorintho 10:13; Mwanzo 22:9-14) Usiambiwe kitu fulani hakiwezekani ukaamini, kwani siku zote ipo njia. Huwezi kushindwa usipokata tamaa.
Jiamini, chukua hatua na usikate tamaa katika kutafuta utatuzi wa tatizo, shida au hali yoyote inayokusumbua katika maisha yako kwani kila muda, kila hali, kila tukio na kila jambo huleta uwezekano na fursa ya kufanya kitu kitakachokuwezesha kusonga mbele na kuleta mabadiliko katika maisha yako.
Kataa kukwamishwa au kuyumbishwa na matatizo na vikwazo toka kwa mwovu shetani ambaye tunashindana naye kila siku na badala yake mwombe Mungu akujaze ufahamu na hekima za Kiroho ili uweze kuzijua na kuzifuata njia zake; (Kutoka 33:13; Zaburi 86:11) Naye atakuonyesha njia na asipokuonyesha atakuwezesha kuifanya njia, kuvivuka vikwazo na kuzishinda changamoto unazokutana nazo. Katika Jina la Yesu Kristo ninakuombea mafanikio katika hili!
There was an error while fetching comments, Please try again later
888888888
mmmmmmmmm
ooooooooo
nnnnnnnnn
ttttttttt
uuuuuuuuu
eeeeeeeee
sssssssss
wwwwwwwww
hhhhhhhhh
rrrrrrrrr
fffffffff
iiiiiiiii
ddddddddd
aaaaaaaaa
yyyyyyyyy
888
mmm
ooo
nnn
ttt
uuu
eee
sss
www
hhh
rrr
fff
iii
ddd
aaa
yyy
month
88
day
88888
GMT
hour
:
minute
second
am
pm
No Comments Yet...